Kumtii Mwenyezi Mungu
Mwenyezi
Mungu anasema;
“Na
anayemtii Mwenyezi Mungu na Mtume Wake, bila shaka amefanikiwa mafanikio
makubwa.”
Al
Ahzab – 71
Kuyashinda matamanio ya
nafsi
Mwenyezi
Mungu anasema;
“Na
ama yule aliyeogopa kusimamishwa mbele ya Mola wake, akaikataza nafsi yake na
matamanio (maovu).
Basi
(huyo) Pepo ndiyo itakayokuwa makazi yake.”
An
Naziat – 40-41
Kuepukana na Moto
Mtume
wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa sallam) amesema;
“Hatoingia
motoni yeyote atakayesali kabla ya kuchomoza juwa na kabla ya kuzama
kwake.(yaani Sala ya Alfajiri na ya Alasiri)”
Muslim
Kuingizwa Peponi
Mtume
wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa sallam) amesema;
“Atakayezisali
(Sala za) ‘baridi mbili’- Alfajiri na Alasiri ataingia Peponi.”
(Zimeitwa
Sala za ‘Baridi mbili' kwa sababu joto hupunguwa nyakati za Alfajiri na Alasiri
na hali ya hewa inakuwa na ubaridi ndani yake).
Bukhari
na Muslim
Kuuangalia uso wa Mwenyezi Mungu mtukufu
Na
hii ni starehe kubwa kupita zote za huko Peponi.
Mtume
wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa sallam) amesema;
“Hakika
nyinyi mtamuona Mola wenu kama mnavyouona mwezi huu, hapana kitakachokuzingeni
msiweze kumuona. Kwa hivyo kama mtaweza msishindwe (na shetani) kusali kabla ya
kuchomoza juwa na kabla ya kuzama kwake, basi fanyeni hivyo”
Bukhari na Muslim
Anakuwa katika hifadhi ya Mwenyezi Mungu na chini
ya ulinzi Wake
Mtume
wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa sallam) amesema;
“Atakayesali Alfajiri (jamaa) yumo katika hifadhi
ya Mwenyezi Mungu.”
Muslim
Kushuhudia kwa Malaika mbele ya Mwenyezi Mungu
kwa wanaosali
Mtume wa Mwenyezi Mungu
(Swallah Llahu alayhi wa sallam) amesema;
“Wanapishana kuja kwenu Malaika wakati wa usiku
na wakati wa mchana. Wanajumuika wakati wa Sala ya Alfajiri na Sala ya
Alasiri,kisha wanapopanda wale waliokesha kwenu, Mwenyezi Mungu huwauliza - juu
ya kuwa ana juwa kila kitu juu yao; “Mumewacha waja wangu wakiwa katika hali
gani?” Na wao hujibu; “Tuliwaacha wakiwa wanasali na tulipowaendea pia walikuwa
wakisali.”
Bukhari na Muslim
Anayesali Ishaa na Alfajiri jamaa anapata thawabu
sawa na aliyesali usiku kucha
Mtume wa Mwenyezi Mungu
(Swallah Llahu alayhi wa sallam) amesema;
“Mwenye kusali Ishaa jamaa sawa na aliyesali nusu
ya usiku. Na mwenye kusali Alfajiri jamaa sawa na aliyesali usiku kucha.”
Muslim
Anaepukana na sifa za wanafiki
Mtume wa Mwenyezi Mungu
(Swallah Llahu alayhi wa sallam) amesema;
“Hapana Sala nzito kwa wanafiki kupita Sala ya
Alfajiri na Ishaa (jamaa), lau kama wangejuwa yaliyomo ndani yake, basi
wangekuja (msikitini kuzisali) hata kwa kusota (kama hawawezi kutembea kwa
miguu yao).”
Bukhari na Muslim
Na kutoka kwa Ibni Omar (RA) amesema;
“Ilikuwa tusipomuona mtu akija kusali Alfajiri na
Isha (msikitini) tukimdhania vibaya.”
Ibni Khuzayma katika Sahihi yake
No comments:
Post a Comment