• Breaking News

    Friday, 6 January 2017

    KUCHORA ‘TATTOO’

    Suali hili wameulizwa maulamaa wengi kama vile Sh. Atiya Saqar na Sh. Yusuf Qaradhawi na wengineo na wamejibu kama ifuatavyo;
    “Kuchora Tattoo (Al Washam) nako ni kuichora ngozi ya mwili ni kitendo kilicholaaniwa na Mwenyezi Mungu na inamuwajibikia mtu aloichora ngozi yake kwa njia ya Tattoo afanye kila jitihada kuiondoa isipokuwa kama kuiondoa huko kutamsababishia madhara au maradhi au yatasababisha kuongezeka kwa michoro hiyo.
    Sala yake inakubaliwa na pia anaweza kuwa Imam ikiwa ametubu kutokana na kosa hilo na ikiwa amejaribu kuitoa tattoo hiyo bila mafanikio au ameshindwa kuitoa kutokana na sababu tulizokwishazitaja.
    Kutokana na yaliyotangulia tunafahamu kuwa mwenye Tattoo hawezi kusalisha wala hawezi kuwalingania watu katika dini ya Mwenyezi Mungu mpaka kwanza atubu kutokana na kitendo chake hicho kisha ajaribu kila njia kuitoa, ama akishindwa kuitoa kutokana na sababu zilizotangulia kutajwa, hapo anasameheka na anaweza kusikilizwa mawaidha yake.
    Na Tattoo imeharamishwa kutokana na hadithi ya Mtume (SAW) isemayo;
    “Mtume (SAW) amewalani wanaochora miili yao (kwa njia ya tattoo) na wanaowachora wenzao…”
    Na katika jumla ya waliolaaniwa katika hadithi hiyo na zilizofanana nayo ni wafuatao;
    “Wanaounganisha nywele zao na wanaowaunganisha, wanaopanua meno yao kwa ajili ya kufanya mwanya, wanaokula riba na wanaolisha na mashahidi wake, wanaochuna nyusi zao nk.”
    Wallahu taala aalam
    Wassalaam alaykum wa Rahamtullahi wa Barakatuh

     


    No comments:

    Post a Comment

    Fashion

    Beauty

    Culture