Suali:
Mtoto aliyenyonya kwa
mama asiyemzaa hawezi kuwaoa ndugu zake
wa kunyonyesha , lakini nataka
kujua jee wale ndugu wa kila
upande ambao wao hawajanyonya pamoja wanafaa kuoana?
Wabillah Taufiq.
Wabillah Taufiq.
Jawabu:
Mtume wa Mwenyezi Mungu (SAW) amesema;
"Waloharamishwa
kuoana kwa
ajili ya kunyonyeshwa ni sawa na walioharamishwa
kuona kwa ajili ya uhusiano
wa nasaba."
Bukhari na
Muslim na wengine
Kwa vile walioharamishwa kuoana kwa ajili
uhusiano wa nasaba ni mama na binti na
dada na khale na shangazi na
mabinti wa dada na mabinti wa
kaka kama alivyosema Mwenyezi Mungu;
"Mmeharamishiwa
(kuoa) mama zenu na watoto wenu
na dada zenu na shangazi zenu
na ndugu za mama zenu na
watoto wa ndugu zenu na
watoto wa dada zenu na mama zenu
waliokunyonyesheni na dada zenu wa kunyonya
na mama wa wake zenu na watoto
wenu wa kambo."
Annisaa – 23
Kwa hivyo aliyenyonyesha
anakuwa mfano wa mama na
kwa ajili hiyo ni haramu
kumuoa na haramu pia kuoa
wote walioharamishwa kumuoa yeye kama ifuatavyo;
Mama aliyenyonyesha
kwa sababu
anakuwa mfano wa mama.
Mama wa
mnyonyeshaji anayekuwa mfano wa bibi.
Mama wa
mume wa mnyonyeshaji
anayekuwa pia mfano wa bibi.
Dada yake anayekuwa mfano wa khale.
Dada wa
mumewe anayekuwa mfano wa shangazi.
Mabinti wake na
binti za wanawe. Nk.
Ndugu wa kunyonyesha ni wale tu walionyonya ziwa la mama pamoja na waliohusiana naye mama yule kama ilivyotangulia kutajwa hapo juu,
na aliyenyonya hawezi kumuoa yeyote
kati ya watoto
wa mama aliyenyonya kwake na hata
wasiokuwa watoto wake ikiwa wamenyonya ziwa lile.
Ama Ndugu wengine wale wasionyonya ziwa la mama yule hao si ndugu wa kunyonya na wanafaa kuoana.
wasiokuwa watoto wake ikiwa wamenyonya ziwa lile.
Ama Ndugu wengine wale wasionyonya ziwa la mama yule hao si ndugu wa kunyonya na wanafaa kuoana.
Natumai itaeleweka.
Wallahu taala aalam
Wassalaam alaykum wa Rahmatullahi wa barakatuh
No comments:
Post a Comment