• Breaking News

    Friday, 6 January 2017

    Janaba

    Suali:
    Jee mtu akioga janaba analazimika kutia udhu japo hataki kwenda kuswali wala kushika msahafu baada ya kuoga?  Au inatosha kuoga tu kiwa amekwisha tia nia ya kuoga janaba bila ya kutia udhuu?
    Pia ni lazima atamke kwa maneno au inatosha kuwa alitia nia tu ya kwenda kukoga janaba?

    Jawabu:

    Anayeoga janaba halazimiki kutawadha, isipokuwa kutawadha ni mojawapo ya Sunnah za kuoga Janaba.

    Ifuatayo ni hukmu ya kuoga janaba;

    Kwanza – Nia - na nia mahali pake moyoni, kwa hivyo kuitamka si katika Sunnah, na maulamaa wengi wanasema kuwa kuitamka nia ni katika uzushi na Muislamu anatakiwa kuepukana na mambo hayo.

    Pili – kuvikosha viungo vyote, yaani maji lazima yakienee kila kiungo cha mwili.

    Mwenyezi Mungu anasema;

    “Na mkiwa na janaba basi ogeni.”

    Al Maidah - 6

    Na akasema;

    “Enyi mlioamini! Msikaribie Sala hali mmelewa mpaka myajue mnayosema, wala hali mna janaba – isipokuwa mmo safarini mpaka mkoge…”,]

    An Nisaa - 43

    Na kukoga maana yake ni kuyaeneza maji juu ya kila kiungo.

     

    Ama kutia udhu ni katika Sunnah za kuoga janaba NA SI KATIKA NGUZO ZAKE na mtu anaweza kuoga bila kutia udhu na kuoga kwake ni sahihi kabisa na wala hapana shaka yoyote ndani yake, ila kama anataka kusali au kufanya ibada inayohitajia udhu  hapo ndiyo anatia udhu.

    Bila shaka kufuata Sunnah ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (SAW) ni bora zaidi, lakini kama nilivyotangulia kusema kuwa SI LAZIMA kutia udhu.


    No comments:

    Post a Comment

    Fashion

    Beauty

    Culture